Simbu arejea nchini, ataja siri ya kung'ara Boston Marathon

Mwanariadha wa Kimataifa wa Tanzania, Alphonce Simbu, leo Aprili 24, 2025 amerejea nchini akitokea Marekani alikokwenda kushiriki mbio za Boston Marathon huku akisema siri ya kufanya vizuri imetokana na jitihada kubwa ambazo amekuwa akifanya kwa kushirikiana na wenzake kwenye mazoezi lakini pia kufuata maelekezo ya mwalimu.