Simba yapewa refa wa 1-0 Sauzi

Mwanaspoti
Published: Apr 22, 2025 15:20:26 EAT   |  Sports

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF), limemkabidhi mwamuzi wa kimataifa kutoka Misri, Amin Omar jukumu la kuchezesha mechi ya marudiano ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Stellenbosch dhidi ya Simba itakayopigwa Aprili 27, 2025 kwenye Uwanja wa Moses Mabhida jijini Durban, Afrika Kusini.