Simba v Berkane ngome mpya, historia mpya ugumu uko hapa!

Mwanaspoti
Published: May 24, 2025 14:51:06 EAT   |  Sports

NI Jumapili ya kihistoria Mei 25, 2025. Macho na masikio ya Afrika yapo Zanzibar kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, ambako kutapigwa fainali ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Simba na RS Berkane.