Simba, Musonda kuna kitu

MAMBO ni moto na muda ni mchache. Simba itakuwa Morocco kukipiga na RS Berkane katika mechi inayotarajiwa kuwa ngumu na yenye hisia tofauti ya Kombe la Shirikisho Afrika, kwani wiki ijayo itakuwa jijini Dar es Salaam kukamilisha ratiba na kukabidhiwa ndoo ya ubingwa.