Polisi yarejea Ligi Kuu Zanzibar

Licha ya vita vya ngumi na midomo iliyotokea leo Jumapili katika mechi ya jasho na damu, maafande wa Polisi wameichakaza Kundemba kwa kuitandika mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Mao B, Mjini Unguja na msimu ujao watacheza Ligi Kuu Zanzibar.