Mzize aitaka Ulaya, awakataa Waarabu

Mwanaspoti
Published: May 09, 2025 14:45:01 EAT   |  Sports

DILI kibao zimetua mezani kwa mabosi wa Yanga kutoka timu zinazotaka kumsajili mshambuliaji Clement Mzize zikiwamo kutoka Afrika Kaskazini, Saudia Arabia na Ulaya, lakini straika huyo mwenye mabao 13 kwa sasa Ligi Kuu Bara amezichomolea za Kiarabu, huku ikielezwa hesabu zake ni kutaka kucheza Ulaya.