Msimu mpya BDL/WBDL, kazi imeanza DonBosco

Mwanaspoti
Published: May 08, 2025 13:12:07 EAT   |  Sports

LIGI ya kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BDL), inatarajia kuanza kesho kwa michezo miwili kupigwa katika Uwanja wa Donbosco Upanga na utaishuhudia UDSM Outsiders itakipiga dhidi ya JKT, huku ikitanguliwa na DB Lioness ikikwaruzana dhidi ya mpinzani wake mkubwa Vijana Queens ikiwa ni michezo ya ufunguzi kwa wanaume na wanawake.