Mbeya City yamnyatia nyota wa Yanga

UONGOZI wa Mbeya City umeanza hesabu za kuiwinda saini ya winga wa Yanga, Farid Mussa ili kuongeza nguvu ya timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara, ikiwa ni katika harakati za kukisuka kikosi hicho ili kilete ushindani zaidi.