Kilichoiua Simba Morocco hiki hapa, yapewa nondo za kuibeba nyumbani

Mwanaspoti
Published: May 17, 2025 21:17:06 EAT   |  Sports

MCHEZO wa fainali ya mkondo wa kwanza Kombe la Shirikisho Afrika baina ya RS Berkane dhidi ya Simba umemalizika nchini Morocco kwa wenyeji kushinda 2-0, hivyo kwa sasa ni kuuendea wa marudiano utakaochezwa Tanzania, Jumapili ijayo huku yakibainika mambo matatu yaliyoigharimu timu hiyo.