KenGold yaipeleka Simba Ruvuma

KENGOLD iliyoshuka mapema hadi Championship kutoka Ligi Kuu Bara iliyoicheza kwa mara ya kwanza msimu huu, imepanga kuipeleka mechi dhidi ya Simba iliyopangwa kupigwa Juni 18 Uwanja wa Majimaji, Songea, mkoani Ruvuma, endapo taratibu za ukaguzi uwanjani hapo zitakamilika mapema.