JKT yachemsha Bara, ila kazi ipo huku

Mwanaspoti
Published: May 09, 2025 14:06:30 EAT   |  Sports

MAAFANDE wa JKT Tanzania kupitia kocha mkuu, Ahmad Ally wamekiri wamechemsha kwa kushindwa kufikia malengo ya Ligi Kuu ya kumaliza ndani ya 5-Bora, lakini kilichobaki kwa sasa wanaelekeza nguvu zote katika Kombe la Shirikisho (FA) ili wakate tiketi ya Kombe la Shirikisho Afrika.