Diddy Combs afungua faili za dhamana tena, hiki ndicho alichosema hakimu

Milard Ayo
Published: Oct 15, 2024 19:36:49 EAT   |  Entertainment

Mkali wa muziki wa hip-hop Sean ‘Diddy’ Combs anatazamiwa kusalia gerezani huku mahakama ya rufaa ikijadili iwapo anafaa kupewa dhamana. Rapa huyo amekuwa akizuiliwa katika gereza la Metropolitan Detention Center huko Brooklyn tangu kukamatwa kwake, huku jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Pili ya Rufaa ikizingatia ombi la timu yake ya kisheria kuachiliwa. Siku […]

The post Diddy Combs afungua faili za dhamana tena, hiki ndicho alichosema hakimu first appeared on Millard Ayo.

Mkali wa muziki wa hip-hop Sean ‘Diddy’ Combs anatazamiwa kusalia gerezani huku mahakama ya rufaa ikijadili iwapo anafaa kupewa dhamana.

Rapa huyo amekuwa akizuiliwa katika gereza la Metropolitan Detention Center huko Brooklyn tangu kukamatwa kwake, huku jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Pili ya Rufaa ikizingatia ombi la timu yake ya kisheria kuachiliwa.

Siku ya Ijumaa, Jaji wa Mahakama ya Rufaa ya Shirikisho William J. Nardini alikataa ombi la Combs kuachiliwa mara moja, ikisubiri uamuzi wa jopo la majaji watatu. Hii ina maana kwamba Combs ataendelea kukaa katika jela ya Brooklyn huku mahakama ikitathmini rufaa ya mawakili wake.

Hakimu pia aliruhusu timu ya wanasheria ya Combs kuwasilisha ombi lao la dhamana chini ya muhuri na marekebisho ya sehemu, kuhakikisha baadhi ya maelezo ya kesi yanabaki kuwa siri.

The post Diddy Combs afungua faili za dhamana tena, hiki ndicho alichosema hakimu first appeared on Millard Ayo.