Dakika 180 zampa faraja David Ouma

BAADA ya kucheza dakika 180 dhidi ya Fountain Gate katika mechi mbili za kirafiki, kocha mkuu wa Singida Black Stars, David Ouma amesema ataendelea kusaka mechi zaidi kujiweka tayari kuikabili Simba katika mechi mbili mfululizo ikiwamo ya Ligi Kuu na nusu fainali ya Kombe la Shirikisho (FA).