Bosi Takukuru afunguka sakata la kipa Fountain Gate

MKUU wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Manyara, Bahati Haule, amesema wameanza rasmi kufuatilia sakata la kipa wa Fountain Gate, John Noble aliyesimamishwa na klabu yake kwa tuhuma za kucheza chini ya kiwango dhidi ya Yanga.