AKILI ZA KIJIWENI: Waziri Palamagamba Kabudi kweli Profesa

JANA Jumatano, kundi lote hapa kijiweni tulikuwa tumekusanyana kusikia na kuona Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi akisoma hotuba ya makadirio ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2025/2026.