Uhuru ataacha deni la ahadi alizotoa kwenye kampeni- Ruto

Taifa Leo
Published: Dec 09, 2021 07:12:34 EAT   |  News

Na WYCLIFFE NYABERI NAIBU Rais Dkt William Ruto amemshambulia Rais Uhuru Kenyatta huku akisema ataondoka mamlakani bila kulipa deni la ahadi alizotoa kwa Wakenya. Dkt Ruto alitumia ziara yake Kisii, kukosoa Rais Kenyatta kuhusu ajenda nne kuu za maendeleo ambazo alisema utekelezaji wake utasalia kuwa ndoto.