Raia wa Nigeria anayeshtakiwa kwa ‘washwash’ apewa masharti magumu ya dhamana

NA RICHARD MUNGUTI RAIA wa Nigeria anayeshtakiwa kumlaghai Mkenya Sh60.4 milioni katika biashara ya ‘washwash’ amepata afueni ya kuachiliwa kwa dhamana kwa vile ameoa Mkenya, huku mwenzake akinyimwa haki hiyo na kuagizwa asalie gerezani hadi kesi inayowakabili isikilizwe na kuamuliwa. Hata hivyo, Alo Ojo, ambaye mkewe na wazazi wake walifika kortini kuthibitisha ni mkwe wao, […]