PAUKWA: Biashara Haramu ya Titi (sehemu 5)

Na ENOCK NYARIKI “KWENU ni wapi?’’ afisa kwenye zamu katika kituo cha polisi alimuuliza Machugachuga. “Masosa. Kwetu ni Masosa katika kaunti ya Nyamira,’’ Machugachuga alieleza. “Umetoka mbali hivyo kuja kufanya biashara ya kuuza pombe haramu?’’ ni kama yule askari alimuuliza, ni kama alimsuta. Machugachuga alijitetea kwamba yeye alikuwa msaidizi wa Titi aliyeimiliki biashara hiyo haramu. […]