Omtatah awasilisha kesi kupinga Mswada wa Fedha 2023

Taifa Leo
Published: Jun 02, 2023 09:55:15 EAT   |  News

NA RICHARD MUNGUTI SENETA wa Busia Okiya Omtatah amewasilisha kesi katika Mahakama ya Milimani jijini Nairobi leo Ijumaa akiiomba itie breki Mswada wa Fedha, 2023. Seneta huyo aliyetofautiana hadharani na Rais William Ruto alipozuru Busia, amesema mswada huo unakiuka Katiba.