Mapato ya wafanyakazi kuendelea kunyofolewa

CECIL ODONGO na RICHARD MUNGUTI WAKENYA, hasa wafanyakazi wanatarajiwa kuendelea kufyonzwa zaidi kufuatia kuwasilishwa bungeni kwa mswada unaopendekeza wafanyakazi kuchangia hazina ya kuwakimu wale ambao wamepoteza ajira. Mswada wa Kubuniwa kwa Mamlaka ya Kuwakimu Wasio na Ajira, 2023 (UIA, Bill) ambao umedhaminiwa na Mbunge wa Ikolomani, Benard Shinali pia unalenga kuwanusuru jamaa za waliopoteza ajira. […]