Mahakama yaambiwa uhusiano wa Maxine Wahome na marehemu Assad Khan ulikuwa wa kelele na vita

NA RICHARD MUNGUTI BINGWA wa Safari Rally Maxine Wahome alikuwa ameolewa na mtu mkorofi, mahakama imeambiwa. Jaji Lilian Mutende alifahamishwa na Chemutai Sogomo Chepkorir, jirani wa Assad Kalulu Khan karibu miaka 10, kwamba “uhusiano wao ulikuwa wa kelele na vita.” “Assad alikuwa na uhusiano mara sita na wanawake na alikuwa akiwachapa kila uchao,” akasema Chemutai aliyekuwa […]