Dorcas Gachagua: Ufukara katika familia nusra usababishe nijitie kitanzi

NA SAMMY WAWERU MKE wa Naibu Rais Rigathi Gachagua, Bi Dorcas Gachagua, amesimulia jinsi nusra ajitie kitanzi kufuatia mahangaiko yaliyozingira familia yake. Akihutubia wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Daystar jijini Nairobi mnamo Septemba 19, 2023, Bi Gachagua alifichua kwamba akiwa mwanafunzi karibu ajiondoe uhai. Aidha alidokeza kwamba jaribio hilo lilichochewa na ufukara uliozingira familia yake […]