Bashungwa awasili shinyanga kukagua athari za mvua

Habari Leo
Published: Dec 08, 2023 10:24:04 EAT   |  Sports

SHINYANGA: Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amewasili mkoani  Shinyanga kwa ziara ya kikazi ambapo amepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme,  Desemba 8, 2023. Katika ziara hiyo, Waziri Bashungwa atakagua miundombinu ya barabara zilizoharibiwa na mvua kubwa za El-nino zinazoendelea kunyesha katika mkoa huo pamoja na maeneo mbalimbali  nchini. Miundombinu hiyo iliyoharibiwa na …

The post Bashungwa awasili shinyanga kukagua athari za mvua first appeared on HabariLeo.

SHINYANGA: Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amewasili mkoani  Shinyanga kwa ziara ya kikazi ambapo amepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Christina Mndeme,  Desemba 8, 2023.

Katika ziara hiyo, Waziri Bashungwa atakagua miundombinu ya barabara zilizoharibiwa na mvua kubwa za El-nino zinazoendelea kunyesha katika mkoa huo pamoja na maeneo mbalimbali  nchini.

Miundombinu hiyo iliyoharibiwa na mvua  ni pamoja na barabara ya Shinyanga – Old Shinyanga, barabara ya Old Shinyanga – Solwa, barabara ya Solwa – Kahama na miundombinu mingine ya barabara katika mkoa huo.

 

The post Bashungwa awasili shinyanga kukagua athari za mvua first appeared on HabariLeo.