Taifa Stars kanyaga twende!

Mwanaspoti
Published: Mar 24, 2023 11:54:46 EAT   |  Sports

HAKUNA namna ni ushindi tu. Mashabiki wa soka wanahesabu saa tu kwa sasa kabla ya kuishuhudia Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars ikishuka Uwanja wa Suez Canal, mjini Ismailia, Misri kuvaana na Uganda ‘The Cranes’, huku ikiwa na kiu ya kuona timu hiyo ikipata ushindi ugenini.