Taifa Stars kanyaga twende!

HAKUNA namna ni ushindi tu. Mashabiki wa soka wanahesabu saa tu kwa sasa kabla ya kuishuhudia Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars ikishuka Uwanja wa Suez Canal, mjini Ismailia, Misri kuvaana na Uganda ‘The Cranes’, huku ikiwa na kiu ya kuona timu hiyo ikipata ushindi ugenini.