Simba katika njia ngumu ya kusaka taji Afrika

Wawakilishi wa Tanzania katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika Simba, wamefanikiwa kutinga hatua ya makundi baada ya ushindi wa jumla wa mabao 4-2 dhidi ya Red Arrows ya Zambia katika hatua ya mwisho ya mchujo ambapo mechi zake za mwanzo zilichezwa Novemba 28 na mechi za marudiano ilikuwa Desemba 5.