Mbrazili aitisha kikao na mastaa

SIMBA imeipiga Pan Africans mabao 4-0 ikiendelea kutengeneza hesabu za kuivaa Power Dynamos ya Zambia kwenye mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, lakini kocha wa timu hiyo, Roberto Oliveira ‘Robertinho’ akiitisha vikao tofauti na wachezaji ili kutengeneza mipango ya kutoka kwa Wazambia.