Dube aanika siri ya 5-0 za Azam FC

AZAM gari lao limewaka kwani kwa sasa wanagawa vichapo kila timu inayokutana nayo kwani jana usiku iliinyoa KMC kwa mabao 5-0, huku mshambuliaji hatari wa timu hiyo kufunga mara mbili na kufunguka siri ya juu ya ushindi mfululizo wa timu hiyo na mzuka walionao kwa sasa kwenye Ligi Kuu Bara.