Wanywaji Pombe wapewa alama tatu, “mdogomdogo, Wajawazito na Madereva”

Milard Ayo
Published: Mar 22, 2023 14:40:55 EAT   |  News

Tanzania Breweries Limited ni kampuni kubwa zaidi ya utengenezaji wa vileo nchini na ni ambayo iko chini ya kampuni Mama AB InBev, imejitolea kukuza utumiaji bora wa pombe na kuathiri desturi za kijamii na tabia ya mtu binafsi ili kupunguza matumizi hatari ya pombe. TBL inajitahidi kufanya Mabadiliko endelevu ya kitamaduni katika Jamii za ndani […]

Tanzania Breweries Limited ni kampuni kubwa zaidi ya utengenezaji wa vileo nchini na ni ambayo iko chini ya kampuni Mama AB InBev, imejitolea kukuza utumiaji bora wa pombe na kuathiri desturi za kijamii na tabia ya mtu binafsi ili kupunguza matumizi hatari ya pombe.

TBL inajitahidi kufanya Mabadiliko endelevu ya kitamaduni katika Jamii za ndani kwa kufanya kila uzoefu na bidhaa za TBL uwe Chanya.

Kampuni hiyo imefanya kazi pamoja na washirika mbalimbali ili kutambua na kuongeza ufahamu wa Pombe kwa watumiaji.

“Kama sehemu ya malengo yetu ya utumiaji bora wa pombe, moja ya mipango muhimu ambayo biashara imejikita ni kuanzisha lebo za ushauri kwa watumiaji ambazo zimejumuishwa kwa hiari katika mkusanyiko wake wote wa bidhaa.

Lebo hizi zitatoa uUuri zitaonyeshwa kwenye lebo za vinywaji pamoja Na vitu vingine vya uendelezaji.” Haya yalisemwa na Mesiya Mwangoka Mkurugenzi wa Greater Africa Sera na Masuala ya Kampuni & LCA Tanzania.

TBL inajivunia kuzalisha na kuuzia bia zao kwa ubora na uangalifu. Kampuni inaamini kuwa ni muhimu kusaidia watumiaji kuelewa jinsi na kwa nini pombe inapaswa kutumiwa ndani ya kikomo. TBL inahakikisha kuwa masoko yao hayalengi watumiaji wa chini ya umri wa miaka 18 na yanadhihirisha ladha nzuri na maadili mema.

Kampuni pia inalenga kuepuka kukuza utumiaji wa pombe au tabia hatari za pombe.

“Viwanda hivi vinavyozalisha vileo vinadumisha zaidi ya ajira milioni 23 kote ulimwenguni, na data kutoka Shirika la Afya Duniani inaonyesha kuwa utumiaji mbaya wa pombe umepungua kote ulimwenguni katika muongo uliopita. Mpango wetu wa siku za usoni kwa utumiaji bora wa pombe Afrika unazingatia zaidi vijana, kwa lengo la kukuza kizazi cha watumiaji waliostaarabika ambao wametawala sanaa ya kunywa pombe hivyo kunywa kwa uwajibikaji na kufanya kila uzoefu na bidhaa zetu kuwa chanya.” Alisema John Blood Mkuu wa masuala ya kisheria na ya kampuni, ABInBev.

Lebo mpya inashughulikia maeneo matatu muhimu ya kunywa kwa uwajibikaji kunywa pombe wakati wa ujauzito, kunywa pombe wakati angali mtoto, na kunywa na kuendesha gari. TBL inatambua kuwa matumizi ya pombe wakati wa ujauzito yanaweza kusababisha matatizo kwa mtoto anayekua, na kunywa pombe kwa watoto ni hatari kwa afya yao na uwezo wa baadaye.

Kampuni pia inatambua kuwa pombe inaweza kupunguza kasi ya majibu na kuharibu usawa, hivyo kufanya kuendesha gari au mashine nzito baada ya kunywa kuwa hatari.

TBL pamoja na ABInBev kiujumla wamesema kuwa lengo lao la utumiaji bora wa pombe ama “Smart Drinking” kote ulimwenguni linalenga kupunguza matumizi mabaya ya pombe kwa 10% ifikapo mwaka 2025, kulingana na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya WHO na UN.

Kampuni imetangaza kampeni yao ya “Mdogo mdogo” kwa ajili ya Lengo la Utumiaji Bora wa Pombe kote ulimwenguni, ambayo inajumuisha programu na mipango inayolenga kubadilisha mitazamo ya watu juu ya unywaji wa pombe.

Elimu juu ya pombe ni sehemu muhimu ya malengo ya endelevu ya kimataifa ya TBL, na kampuni inalenga kubadilisha tabia hatari za kunywa pombe kwa kuchukua hatua za kubadilisha mila za kijamii kuhusu matumizi ya pombe. TBL inaamini kuwa kila uzoefu na bia inapaswa kuwa chanya, na kampuni imejitolea kuboresha juhudi zake na mazoea ya biashara. TBL inalenga kushiriki kile wanachojifunza na wengine ili kusaidia kutatua tatizo tata la utumiaji mbaya wa pombe.