Ramaphosa anatibiwa corona

Milard Ayo
Published: Dec 13, 2021 07:55:12 EAT   |  News

Rais wa Afrika Kusini Cyrill Ramaphosa amebainika kuwa na Covid 19 leo Jumapili December 12,2021 na sasa anapatiwa matibabu, taarifa iliyotolewa na Serikali ya Afrika Kusini inasema Ramaphosa hayupo kwenye hali mbaya lakini afya yake inafuatiliwa kwa ukaribu na Wahudumu wa Afya kutoka Jeshi la Afrika Kusini.

Rais wa Afrika Kusini Cyrill Ramaphosa amebainika kuwa na Covid 19 leo Jumapili December 12,2021 na sasa anapatiwa matibabu, taarifa iliyotolewa na Serikali ya Afrika Kusini inasema Ramaphosa hayupo kwenye hali mbaya lakini afya yake inafuatiliwa kwa ukaribu na Wahudumu wa Afya kutoka Jeshi la Afrika Kusini.

Ramaphosa ambaye amechanjwa chanjo zote zinazohitajika kwa sasa amejitenga Cape Town na majukumu yake yanatekelezwa kwa muda na Naibu Rais David Mabuza, wote waliokutana na Rais huyo siku za karibuni wameshauriwa kupima Covid ili kujua hali zao.