Mpishi wa timu ya Arsenal Bernice Kariuki astaafu

Milard Ayo
Published: May 30, 2023 09:54:14 EAT   |  Sports

Bernice Kariuki, Mkenya mwenye maono makubwa ambaye anahudumu alihudumu  kama mpishi wa binafsi wa timu ya kwanza ya klabu ya London, Arsenal. Huku baadhi ya mashabiki wapenzi kabisa wa Arsenal wakiwa na ndoto ya kukutana na wachezaji wanaowaenzi siku moja, Bernice yeye alikuwa ana nafasi ya kipekee ya kuwapikia chakula. Upendo wake kwa mapishi ulimsaidia […]

Bernice Kariuki, Mkenya mwenye maono makubwa ambaye anahudumu alihudumu  kama mpishi wa binafsi wa timu ya kwanza ya klabu ya London, Arsenal. Huku baadhi ya mashabiki wapenzi kabisa wa Arsenal wakiwa na ndoto ya kukutana na wachezaji wanaowaenzi siku moja, Bernice yeye alikuwa ana nafasi ya kipekee ya kuwapikia chakula.

Upendo wake kwa mapishi ulimsaidia kupata kazi katika mahoteli ya kifahari nchini Uingereza kama mpishi na amewahi kufanya kazi na mahoteli kama vile The Lanesborough, The Dorchester na The Waldorf Hilton London miongoni mwa nyingine. Lakini kile anajivunia zaidi kwani alikuwa mpishi binafsi wa timu ya  Arsenal, nafasi aliyopata wakati Gunners walipomteua Mikel Arteta kuwa kocha wao.

Akihudumu chini ya uongozi wa Darren Taylor, Mpishi Mkuu wa Arsenal, jukumu lake Bernice lilikuwa ni kuwapikia wachezaji wa timu  na wanachama wa ushauri na uongozi wa timu hiyo.

Sasa Bernice Kariuki ametangaza kuacha kazi Arsenal, timu ya soka ya Ligi Kuu ya Uingereza baada ya miaka miwili.

Chini ya uongozi wa mpishi mkuu wa Arsenal, Kariuki amekuwa mpishi wa wachezaji wa kikosi cha kwanza, uongozi na benchi wataalamu wa ufundi la klabu hiyo.

Akitangaza kuondoka kwake kupitia mtandao wa kijamii Jumapili, alisema kampeni ya Arsenal 2022/2023 ndio ilikuwa mwaka wao mzuri zaidi,akibainisha kuwa ilikuwa jambo la kufurahisha kufanya kazi kwa klabu hiyo.

“Siku ya mwisho inashamiri Ilimaliza msimu kwa kishindo! Bora zaidi!!! Arsenal… Arsenal… Arsenal.. 2020/2023 msimu bora zaidi kuwahi kutokea ninapoondoka kama mpishi wa kujivunia, imekuwa heshima kufanyia kazi klabu bora zaidi duniani… kwa unyenyekevu!” aliandika.

Mpishi huyo pia aliwashukuru Wakenya kwa kumuunga mkono, na kuongeza: “Baraka zaidi katika kazi yangu ijayo ni kama ndoto ya kifalme… Asanteni sana hasa nchi yangu.”

Kariuki alijiunga na Arsenal katikati ya 2021, baada ya Mikel Arteta kuteuliwa kama meneja wa Arsenal, kama mpishi wa kibinafsi wa kikosi cha kwanza