Kuwa shuhuda wa Simu za kufungia mwaka Infinix Hot 11 na Hot 11 play

Milard Ayo
Published: Dec 13, 2021 12:00:09 EAT   |  General

Wahenga walisema hayawi hayawi sasa yamekuwa. Hapo awali zilizuka fununu nyingi kuhusu toleo jipya la Infinix, ikisemekana kampuni ya simu Infinix mbioni kuachia model ya kwanza ya HOT series kuwa na camera ya MP 50 na inch 6.82 kioo ambacho ni ang’avu kuwahi kuwepo kwenye series hiyo ya HOT.

Wahenga walisema hayawi hayawi sasa yamekuwa. Hapo awali zilizuka fununu nyingi kuhusu toleo jipya la Infinix, ikisemekana kampuni ya simu Infinix mbioni kuachia model ya kwanza ya HOT series kuwa na camera ya MP 50 na inch 6.82 kioo ambacho ni ang’avu kuwahi kuwepo kwenye series hiyo ya HOT.

Lakini mapema ya leo kupitia kurasa ya @infinixmobiletz kampuni hiyo imetangaza rasmi ujio wa Infinix HOT 11 na HOT 11 play na kwa kumujibu wa chanzo hicho modeli hizo mbili kuzinduliwa rasmi kesho kwa kushirikiana na kampuni ya mawasiliano Tigo Tanzania.

Kwa mujibu wa vyazo vya awali alinukuliwa mkuu wa bidhaa za Infinix Bwana Eric Zheng, akisema “Tumetengeneza HOT 11 na HOT 11 play kwa kuzingatia matumizi ya mtumiaji kwa kuipa simu chipset ya hali ya juu ya G37 kwa ajili ya utendakazi kwa umahiri usio na kikomo ikishirikiana kwa ukaribu zaidi na uang’avu na wepesi unaotokana na resolution ya FHD+ na nyuzi 90Hz zenye kuifanya simu kurudi katika speed ya awali kila baada ya utumiaji pasipo kupitwa na tukio lolote kutokana na na teknolojia ya Super Charge na kamera iliyojawa program za kisasa kama snapchat na nyenginezo zenye kuifanya modeli hii kuwa ya kipekee”.

Sifa nyengine za simu hizi bado kufahamika mimi na wewe tuungane nao Mubashara kupitia @infinixmobiletz kufahamu mengi zaidi kuhusu Infinix HOT 11 na HOT 11 play.