Copco yatupwa nje kombe la FA, yabamizwa 5-0
YANGA leo ilikula kiporo cha mechi za Kombe la Shirikisho kiulaini baada ya kuifumua Copco ya Mwanza kwa mabao 5-0, huku nyota mpya wa kikosi hicho, Jonathan Ikangalombo ‘Ikanga Speed’ akishindwa kuanza kuitumikia timu hiyo baada ya kuanzishwa jukwaani na Kocha Sead Ramovic.