Wito watolewa kuwe na sheria madhubuti kulinda ujuzi na ubunifu wa wanachuo
Na LAWRENCE ONGARO HUKU wanafunzi wa vyuo vikuu wakiendelea kuonyesha ubunifu ili kuzima ukosefu wa ajira, baadhi ya kampuni kubwakubwa zinajaribu kuwapunja. Naibu Chansela wa Chuo Kikuu cha Zetech mjini Ruiru Dkt, Njenga Munene, aliwatetea wanafunzi wabunifu aliosema wengi hunyanyaswa na kampuni kubwa. Akihutubu katika hafla ya maonyesho ya ubunifu iliyohudhuriwa na zaidi ya wabunifu […]