TAHARIRI: Magavana wasifiche maovu ya watangulizi wao
NA MHARIRI MAGAVANA walioingia mamlakani baada ya Uchaguzi Mkuu wa Agosti, wanafaa kutendea haki wananchi kwa kusaidia kulinda mali zote za umma. Katika baadhi ya kaunti ambazo zilipata magavana wapya, viongozi hao waliingia kwa mbwembwe tele wakionyesha nia ya kuleta mabadiliko. Mabadiliko makuu yalilengwa katika sekta ya fedha na ajira za wafanyakazi. Kuna magavana waliounda […]