Mwili wa mlinzi wapatikana ndani ya darasa
NA GEORGE MUNENE MWILI wa mlinzi wa Shule ya Msingi ya Kanjuu, eneobunge la Gichugu, Kirinyaga, jana Jumamosi ulipatikana ndani ya darasa ambalo halitumiki kwa shughuli za masomo. Wanafunzi ambao walikuwa wakicheza karibu na darasa hilo waliona mwili wa mlinzi huyo Peter Chomba Ndumbi, 62.