Mtaala wa CBC: Wadau watoa maoni mseto
NA WAANDISHI WETU WAZAZI wanaotoa maoni mbele ya jopo kazi linalochunguza ufaafu wa mtaala wa Utendaji na Umilisi (CBC), wamependekeza mageuzi kadhaa kabla ya wanafunzi kujiunga na shule za sekondari ya chini. Katika Kaunti ya Nyandarua, wazazi waliambia jopo lililoundwa na Rais William Ruto, kwamba watoto wao ni wachanga kuhudhuria sekondari ya chini katika shule […]