Nabi afuata dawa ya Mazembe
KOCHA wa Yanga, Nasreddine Nabi ametimka nchini kwenda Ulaya, huku akitoa salamu ambazo hazitakuwa njema jijini Lubumbashi, DR Congo, akisema hesabu zake sasa ni kumaliza na ushindi katika mechi ya mwisho ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.