Dabi ya Wakata Miwa, Makocha watambiana
DABI ya Wakata Miwa, Kagera Sugar na Mtibwa Sugar itapigwa kesho katika Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza kuanzia saa 8 mchana huku makocha wa timu hizo wakitambiana kila mmoja akizitaka pointi tatu ili kikosi chake kiendelee kukwea juu katika msimamo wa Ligi Kuu Bara.